Nguu za Jadi - Sifa na umuhimu wa wahusika
SIFA NA UMUHIMU WA WAHUSIKA. 1. MANGWASHA Huyu ndiye mhusika mkuu katika riwaya. Ni mkewe Mrima na mhazili wa Chifu Mshabaha. Hulka za Mangwasha: Mvumilivu Mangwasha anavumilia matatizo mengi ndani ya ndoa yake yanayotokana na ulevi wa mumewe. Hata baada ya kukimbiwa na Mrima, anavumilia mateso mengi ya ukosefu wa pesa za kuwatunza wanawe, kukiwemo pia kejeli za Sagilu. Mzalendo Mangwasha anaonyesha uzalendo pale anapotamani kukutana na viongozi wa Matuo ili amani iweze kudumishwa nchini. Anajali sana mustakabali wa nchi ya Matuo hasa pale anapowaona watoto na vijana wakiteseka bila matunzo mema ya wazazi wao au hata ajira. Mwenye matumaini Haonekani kufa moyo bali anaonyesha matumaini pale Chifu Mshabaha anapomdharau na kumdhalilisha akiwa kazini. Anaonyesha matumaini pale anapohangaika kutunza wanawe dhidi ya mateso aliyokuwa akipitia alipokimbiwa na Mrima. Anapochomewa nyumba yake pamoja na wenyeji wa Matango havunjiki moyo bali anakuwa na tumaini. Jasiri Mangwasha anaonyesha ujas