Posts

Showing posts from June, 2023

Nguu za Jadi - Dhamira ya mwandishi

                                                                                 Dhamira ya mwandishi Dhamira ni shabaha,nia, kusudi, au lengo kuu la kazi ya fasihi. Aidha inaweza kuwa ni shinikizo kuu liliopelekea utunzi au uwasilishaji wa kazi za kisanaa fasihi ikiwemo. Katika riwaya ya Nguu za Jadi, mwandishi anamulika masuala yafuatayo: a)  Anakemea ukabila uliosakini katika jamii na unaodumaza maendeleo ya nchi. b)  Anatuonyesha jinsi ufisadi unavyoweza kubomoa asasi za kijamii na kufukarisha wananchi kiasi cha kutoweza kujiendeleza kimaisha. c)  Anatuonyesha jinsi ufisadi unavyoweza kusambaratisha uchumi wa nchi hasa pale unapochangiwa na uongozi mbaya kama vile ilivyotukia katika riwaya ya Nguu za Jadi.   MAUDHUI KATIKA RIWAYA YA NGUU ZA JADI Ukabila/Unasaba Ukabila ni hali ya kupendelea mtu, watu au Jamii fulani kutokana na misingi ya jamii/kabila alimotoka. Upendeleo huu huweza kuhusisha mambo mengi kama vile ajira, elimu, makazi, vyeo, na kadhalika. Katika riwaya hii, ukabila

Nguu za Jadi - Jalada na ufaafu wa anwani

  Jalada na Ufaafu wa Anwani: Riwaya ya Nguu za Jadi Katika jalada la riwaya ya Nguu za Jadi, kuna vitu anuwai vinavyoonekana, na vinaweza kuwa na fasiri mbalimbali kwa wasomaji tofautitofauti. Vitu vilivyopo kwenye mchoro wa jalada hilo ni: a) Picha ya mwanamume mzee aliyeketi na anayeonekana kama anayemzungumzia mvulana. Ni wazi wamefunikwa kwa kiwango na giza. Hii inaweza kuchukuliwa kama ishara ya mtoto wa kiume ambaye ametanzwa na matatizo katika jamii ya Matuo. Mtoto wa kiume hajapewa hadhi anayostahili katika jamii hii, aidha hajawajibika inavyostahiki kama inavyoonekana baadaye kwenye riwaya yenyewe. b) Mbele ya picha ya mwanamume anayemzungumzia mvulana kuna uwanja usiokuwa na mimea, pengine kutokana na uharibifu wa mazingira, jambo ambalo pia linajitokeza na kufanywa na viongozi na kusababisha utupu ndani ya riwaya. c) Mbele huko kuna miti ambayo imefunikwa na giza kiasi, ambayo inaweza kuchukuliwa kuwakilisha matumaini yaliyonyimwa nafasi ya kujitokeza vizuri lakini baadaye

Nguu za jadi - dhamira ya mwandishi

  DHAMIRA YA MWANDISHI Dhamira ni shabaha,nia, kusudi, au lengo kuu la kazi ya fasihi. Aidha inaweza kuwa ni shinikizo kuu liliopelekea utunzi au uwasilishaji wa kazi za kisanaa fasihi ikiwemo. Katika riwaya ya Nguu za Jadi, mwandishi anamulika masuala yafuatayo: a)  Anakemea ukabila uliosakini katika jamii na unaodumaza maendeleo ya nchi. b)  Anatuonyesha jinsi ufisadi unavyoweza kubomoa asasi za kijamii na kufukarisha wananchi kiasi cha kutoweza kujiendeleza kimaisha. c)  Anatuonyesha jinsi ufisadi unavyoweza kusambaratisha uchumi wa nchi hasa pale unapochangiwa na uongozi mbaya kama vile ilivyotukia katika riwaya ya Nguu za Jadi.   MAUDHUI KATIKA RIWAYA YA NGUU ZA JADI Ukabila/Unasaba Ukabila ni hali ya kupendelea mtu, watu au Jamii fulani kutokana na misingi ya jamii/kabila alimotoka. Upendeleo huu huweza kuhusisha mambo mengi kama vile ajira, elimu, makazi, vyeo, na kadhalika. Katika riwaya hii, ukabila unadhihirika ifuatavyo: a)  Wakule ni jamii inayoonyesha ukabila; wao ndio wen